Droo ya AFCON U20 2025 Kufanyika Kesho

Filed in Michezo Bongo by on February 12, 2025 0 Comments

Droo ya AFCON U20 2025 Kufanyika Kesho | Tanzania inasubiri hatima yake. Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) litaandaa droo rasmi ya mashindano ya AFCON U-20 2025 2025 kesho, 13 Februari 2025, kuanzia 9:25 p.m. Tanzania ni miongoni mwa mataifa ambayo yamefuzu kushiriki michuano hiyo muhimu ya vijana wa U-20 ya Afrika.

Droo ya AFCON U20 2025 Kufanyika Kesho

Droo hii ndiyo itakayoamua hatima ya kila timu kwa kupanga makundi rasmi ya mashindano, yatakayotoa nafasi kwa timu za juu kutinga hatua ya mtoano. Tanzania inatarajia kupata kundi pinzani lenye nafasi ya kusonga mbele katika michuano hiyo.

Tanzania kwa mara nyingine inaingia kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 20 ikiwa na matumaini makubwa ya kufanya vizuri na kushindana na mataifa makubwa ya soka barani Afrika. Mashabiki wa soka wanaisubiri kwa hamu droo hii ili kujua Ngorongoro Heroes itakutana na nani katika harakati za kuwania ubingwa wa Afrika kwa vijana.

Mataifa Yaliyofuzu kwa AFCON U20 2025

Mbali na Tanzania, mataifa mengine 13 yaliyofuzu kushiriki michuano hii ni:

Droo ya AFCON U20 2025 Kufanyika Kesho

Droo ya AFCON U20 2025 Kufanyika Kesho

Côte d’Ivoire (Wenyeji)
DR Congo
Misri
Ghana
Kenya
Morocco
Nigeria
Senegal
Sierra Leone
Afrika Kusini
Zambia
UNIFFAC (Timu 2)

Pendekezo La Mhariri:

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *