Makundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco

Filed in Michezo Bongo by on February 13, 2025 0 Comments

Makundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco | SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetangaza makundi rasmi ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON U-17) 2025 zitakazofanyika nchini Morocco.

Droo hiyo imezua shangwe kubwa miongoni mwa mashabiki wa soka barani Afrika huku kila timu ikianza kujiandaa na mchuano huo muhimu wa vijana.

Makundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco

Mashindano haya yatahusisha timu 16, ambazo zimegawanywa katika makundi manne kama ifuatavyMakundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco/v:

Group A

  • ๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฆ Morocco (Mwenyeji)
  • ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ฌ Uganda
  • ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ Tanzania
  • ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฒ Zambia

Tanzania imepangwa kwenye kundi A pamoja na mwenyeji Morocco, timu yenye historia nzuri katika mashindano haya. Uganda na Zambia pia ni wapinzani wenye nguvu ambao wanatarajiwa kuleta ushindani mkubwa.

Group B

  • ๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ซ Burkina Faso
  • ๐Ÿดโ€โ˜  UNIFFAC 1
  • ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฆ South Africa
  • ๐Ÿ‡ช๐Ÿ‡ฌ Egypt

Egypt na South Africa zinachukuliwa kuwa timu zenye uzoefu mkubwa, huku Burkina Faso nayo ikijulikana kwa vipaji vya vijana wenye uwezo mkubwa wa kushindana.

Group C

  • ๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ณ Senegal
  • ๐Ÿ‡ฌ๐Ÿ‡ฒ The Gambia
  • ๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ด Somalia
  • ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ณ Tunisia

Senegal na The Gambia zinafahamika kwa kuzalisha vipaji bora barani Afrika, lakini Somalia na Tunisia pia wanatazamiwa kutoa upinzani mkali.

Makundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco

Makundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco

Group D

  • ๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฑ Mali
  • ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡ด Angola
  • ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ Cรดte d’Ivoire
  • ๐Ÿดโ€โ˜  UNIFFAC 2

Mali na Cรดte d’Ivoire ni miongoni mwa timu zenye historia kubwa katika soka la vijana, huku Angola nayo ikiwa na vipaji vikubwa vinavyoweza kushtua wapinzani wao.

Tanzania kwenye Fainali za Mataifa ya Afrika za U-17 2025

Tanzania imerejea kwenye michuano hiyo baada ya juhudi kubwa kutoka kwa wachezaji wake chipukizi. Kuwa kundi moja na timu za Morocco, Uganda na Zambia ni changamoto, lakini pia ni fursa kwa Serengeti Boys kuonesha umahiri wao kwenye michuano ya kimataifa.

Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Morocco 2025, inatarajiwa kuwa michuano ya kusisimua, timu zote zikilenga kufanya vyema na kufuzu kwa hatua ya mtoano. Tanzania ikiwa ni miongoni mwa washiriki, imepata fursa ya kuweka historia na kufanya vyema dhidi ya wapinzani wao/Makundi ya AFCON U-17 2025 Tanzania Kundi Moja na Morocco.

Pendekezo La Mhariri:

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *